www.guthriememorial.org

 


 

Articles


JIHADHARI NA MTEGO WA ZAKA

DHIHIRISHO LA UFALISAYO KATIKA MAFUNDISHO YA MAKANISA KUHUSU ZAKA NA: Dkt Fillmer Hevener….

DIBAJI

 

Kama vile kila mtu ana alama za vidole za kipekee, kila mtu pia ana ubongo wa kipekee. Ni huu upekee unaotufanya wale tulio.

Chukulia kwa mfano upekee wa ubongo wako ulifanya tiba kwa ugonjwa wa binadamu ulioogofiwa, Je, itakuwa jukumu lako kwa binadamu wenzako kudhihirisha tiba hiyo? Utashiriki kipande hicho cha upekee wako na wengine? Lakini inafaa hivyo ikiwa wapania kupunguza usumbufu!

Wakati unafichua udhalimu unaofanyiwa binadamu wenzako ni wajibu wako kudhihirisha udhalimu huo? Musa alihisi inamfaa, Jefferson alijua inamfaa, Ghadi alidhamiri inamfaa, Joan wa Are kwa ukweli aliamua inamfaa. Tunapoona wanadamu wakipungua tuna jukumu la kufaamisha ulimwengu mabaya haya.

Hata hivyo kuna tofauti kubwa kati ya kudhihirisha tiba kwa ugonjwa na kudhihirisha makosa yaliyopatikana kuwa ukweli. Kufanya ijulikane ya kwanza ni uchangamfu, kufanya ijulikane ya pili huhitaji ushupavu kwa wale watu mashuli yaliyoendelea kwa kupunga wengine hukereka kuona mapato yao yakikatizwa. Kwa hivyo ilivyokuwa siku za utumwa katika karne ya kumi na tisa; ndivyo ilivyo hata karne hii ya ishirini na moja! Ndivyo itakavyokuwa wakati ghadhabu inayotarajiwa, ya wapokezi fulani wa zaka watakaposoma kijitabu hiki na kumtusi mwandishi wake kuwa mwongo, mtovu wa nidhamu na hulka njema na mtaja jina la Mungu kwa uwongo.

Lakini kunaweza kuwa wahubiri fulani wasio na habari wapokeao zaka wasiojua mafundisho ya Biblia kuhusu maudhui ya zaka na usaidizi wa kanisa, lakini baada ya kusoma somo hili hata hawa wasio na habari hawataweza kujitetea kwa kutojua. Hata hivyo ni mkuu wetu aliyesema “Wamebarikiwa wakati binadamu watawatusi na kuwadhulumu na kusema kila aina ya uwongo kuwahusu, kwa jina langu. Furahi kwani ni mkuu ujira wenu mbinguni ilinyokuwa kwa watabiri walioishi mbele yenu (Matayo 5:11,12).

Somo hili linawalenga wakristo wote wanaohitaji kujua mafundisho ya Biblia kuhusu zaka.



ZAKA: BIASHARA KUU .

(Ulaji wa kikanisa au uhitaji wa binadamu?)

Zaka ni chanzo cha mapato kwa mashirika mengi ya makanisa ya kikristo. Katika mashirika ya pwani ilichapisha mapato ya zaka ya mwaka. Kongamano hili lenye wat takribani 22,500 liliripoti mapato yake ya zaka ya takribani pauni 18,000. Haya ni kama pauni 800 kwa kila mtu. Lakini kumbuka hii haijumuishi matoleo wanachama waliopeana kwa makanisa yao na kongamano kwa kuongezeka kwa zaka.

Nikiwa nimekaa katika kamati mbili za makongamano ya kikristo kwa jumla ya miaka kumi na mitan, ninaweza kusema kwa ukweli kwa maoni yangu, kila moja la mashirika haya lilipata fanaka kutokana na zaka na wanachama, yalioangaziwa kila mara.

Jambo la tatu lilioangaziwa lilikuwa kuongezeka kwa mtaji, ujenzi wa makanisa kwa uzingatifu. Kanisa lilianzisha mfuko maalum wa kukopa makanisa pesa za kujengea majengo mapya na kukarabati yale yaliyochakaa. Lakini katika hili kanisa hata kama wanakanisa hulipia ardhi na jengo, shirika la conference, si wanakanisa wanaolipa madeni, huwa na hati ya umilki mali yote ya kanisa.

Wakati wa huduma hii ya kujitolea katika kamati zote mbili siwezi kukumbuka kamati yoyote ya conference ikizungumzia vile itakavyosaidia wajane, wakiwa na maskwota katika mipaka yake. Mkazo mkubwa ulitiliwa uendeshaji wa hospitali hata hivyo.

Pengine sababu kubwa isiyosemwa kwa kutilia maanani hospitali na kupuuza makao ya yatima, wajane na maskwota ni kwa kuwa hospitali huleta faida ilhali haya mengine yanadhaniwa kupunguza pesa za kanisa.

Unauliza (kwa nini hukusema wakati huo?) Wacha niwahakikishie kuwa wakati huo sikujua vizuri juu ya mafundisho ya kanisa lilikuwa linanifundisha injili ya Biblia. Hata hivyo nilipoujua ukweli mwenyewe kupitia kwa kusoma Biblia maombi na utafiti, sasa ninajaribu kurekebisha makosa yangu ya miaka iliyotangulia.

Tusaidie ulaji huu wa kikanisa au mahitaji ya kibinadamu?



Yalioyangaziwa

Utatifiti huu uta: (1) Leta mafundisho ya Bibilia kuhusu zaka, haja na kazi yake. (2) Onyesho kuwa kanisa yeyote ya kikristo itumiayo zaka kama uchumi wqke inatakikana kuwasilisha mpango huu kama jaribio la kibiashara ya kikristo, sio kupitia kwa neno la Mungu.

Tafadhali kumbuka kuwa kando na historia husika mwandishi huyu hutumia vianzao vya Biblia. kiwango cha imani ya mkristo lazima kiwe maandiko sheria na ushuhuda wala sio Papa Mtabiri, Mkuani, Mfalme, kamati.

Kitabu cha kanisa, utamaduni au chanzo chochote cha kibinadamu kwa kuwa “……………. Kama wanazungumza sio kulingana na neno hili, ni kwa sababu mwangaza ndani yao (Isayo 8:20).

Ikiwa tu imetajwa, vifungo vyote vya Biblia vilivyotumika hapa ni kutoa kwa Biblia ya Mfalme Yakobo.



SURA YA KWANZA

KUTOA ZAKA KATIKA AGANO LA KALE

Kulingana na (Walawi 27:32) zaka ni fungu la kumi la faida ya mtu. Katika (kumbukumbu la torati 14:28) Waisraeli waliambiwa walete zaka ya “nyongeza”.

Ni muhimu kukumbuka kuwa kutoa zaka kulikuwepo tangu kabla historia ya Israeli.

Katika sherehe za wasemite na indo-German waliokuwa hawamjui Mungu. Iliaminika kuwa kama miungu haingepokea haki yao hawangepeana baraka zao mwaka uliofuata James Hasstings, Kamusi ya Biblia 1005.

Pia, zaka haikuwa kawaida ikikusanywa kwa ajili kutoa zaka kulikuwa miongoni mwa watu wa zamani “Kwa sababu zao na zisizo za kikanisa…..” Kamusi ya Biblia ya Seventh-Day Adventist, 1127.

Zaka, ikihitajika chini ya amri ya Musa.

Ukisoma zaka yote ilivyowashilishwa katika Biblia, utagundua kuwa kutoa zaka kumetajwa kwa mara ya kwanza katika (Mwanzo 14:17-24). Pale Abraham anapozungumziwa “anayetoa” toleo la fungu la kumi kwa Melchizedek, Mfalme wa salami.Walakini “tunalipa”, wajibu, lakini “tunatoa”, zawadi kwa hiari. Hapakuwa na sheria ya kutoa zaka katika neno la Mungu akimtaka Abraham amlipe Melchizedek zaka kutokana na madhara ya vita.

Ni wazi, kutoa zaka kulijumulishwa katika amri ya Musa, pamoja na matoleo ya kuchoma, kafara, ahadi na upashaji tohara.

(Kumbukumbu la torati sura 11, 12, 14 na 26 Walawi sura 12) “Chini ya mfumo wa Walawi, Mungu akidhanisha ………….. Zaka ………….” Kamusi ya Biblia S.D.A, 1127.

Kwa sababu Abraham “alitoa” zaka kwa Melchizedek kabla ya Musa na sheria za siku zake, baadhi ya kawaida.

Kuongezea baadhi ya makanisa hudadili kuwa Abraham alimlipa vile maandishi yasemavyo sufiri nukta moja ya uharibifu wa kivita wala sio moja juu ya kumi. Walawi walipata moja juu ya hamsini ya uharibifu wa kivita wal sio moja juu ya kumi. Sheria iliyohusu uharibifu wa kivita haikuhusikana na zaka (Hesabu 31:27-28) sasa Musa katika mwanzo alikuwa anaandikisha sheria ya jumla ya kutoa zaka wakati wa Abraham. Kwa nini ajiondoe kwa sheria hii miaka mia nne baadaye? Zawadi ya Abraham ilikuwa ya kujitolea, toleo la shukrani bila nyogeza wa upungufu.

Ni kweli kuwa kutoa zaka ilikuwa sehemu ya sheria zilizoandikwa (kumbukumbu 14:22-29 na 26:12) lakini wafalisayo wakauchukulia kuwa kulikuwa ni sheria ya kawaida ya kutoa zaka wakati wa Abraham hufuatwa mara tu baada ya mtu kupashwa tohara. Kutahiriwa kulikuwepo kabla ya Musa (Mwanzo 17:10) na kulijumlishwa katika sheria zingine kama kutoa zaka. (Walawi 12:3) Hata hivyo tunavyoona katika wakolosai 2 – 16, Paulo anasema kuwa kifo cha Yesu kilimaliza sheria za Musa (Waibrania 9:8 - 11) ikijumuisha tohara wagalatia 5:6 kwa hivyo hata kama tohara na zaka vilikuwepo kabla ya Musa na kuandikwa kwa sheria zake, hili halikufanya matendo haya kawaida.



LENGO NA MATUMIZI YA ZAKA

Kumbukumbu 14 Waziwazi na inatoa lengo la zaka na vile ilivyotumika. Nukuu za vifungu 22 – 29 inaonyesha hivi.

Fungu 22 – Waisiraeli waliagaziwa kutoa zaka kwa nyongeza ya mazao yao kila mwaka.

Fungu 23 – Mkulima na familia yake walikuwa watumie zaka katika sherehe na katika kumheshimu Mungu aliyebariki bidii yao katika mwaka uliotangulia na aliyependekeza mahali pa dhabihu, walikuwa watoe mafuta, mzabibu na wanyama.

Fungu 24 – 26 ikiwa mahali pa kutolewa dhabihu palikuwa mbali basi mkulima na familia yake aliusa na kutoa zaka? Yawezekana kuwa hajawahi haja yake kwa kuogopa uwongo wake. Je? Wanaogopa kulewa kwenu jinsi Mungu alivyoagiza zaka itumike wakati wa walawi?

Fungu 27 – Waliolinda madhabahu walihudumu kama wahubiri walikuwa wapokee baadhi ya zaka sio kiwango fulani kwani hawakuwa wamiliki mali, ardhi ingawa baadaye tukisoma maagizo ya Paulo katika agano jipya kuhusu wahubiri tutaona kuwa mfumo wa wahubiri wa siku ya Musa ulifutiliwa mbali wakati yesu alipokuwa mhuburi mkuu wa wote walioamini. Kwa hivyo mhubiri wako hachukui nafasi ya mhubiri wa walawi, aliyechinjiwa kafara na akawa mpatanishi kati ya mtenda dhambi na Mungu. Vile tutakavyoona Paulo anafundisha kuwa kifo cha Yesu kilichukua mahali pa kafara ya wanyama na Yesu pekee ndiye aliyehudumu kama mpatanishi wa binadamu na Mungu. Katika Matayo 25, tutaona Yesu pia akituambia tutakavyo mpatia mhubiri wetu mkuu na jinsi ya kumtumikia, binafsi.

Fungu 28 – Katika mwisho wa mwaka wa tatu wa mfuatano was sabato Waisraeli walikuwa walete zaka ya nyongeza na walihifadhi katika hifadhi zao.

Fungu 29 – Tena walikuwa wapate sehemu ya zaka hili zilikuwa zigharamie mahitaji ya wakimbizi, wajane na yatima, walioishi vijijini mwa watoa zaka.

Fananisha fundisho hili la Biblia na lile la Ellen White aliyeandika. Mmoja hufikiria kuwa zaka inaweza kutumika katika kazi za shule. Na wengine hufikiria kuwa watahitaji uungwaji mkono watakikana kusaidiwa na zaka. Lakini kosa kubwa hutendwa wakati zaka haitumiki kwa lengo la kuwasaidia wahuburi upigiaji mstari ni wangu ushuda chapisho la 9,248 – 249.

Pia alifundisha kuwa zaka isitumike kuwasaidia (counses of stewardship 103) kwa nini Bi. White haungi mafundisho ya Biblia, kutumia zaka kuwasidia.

Baadhi ya watu wamesema kuwa kumbukumbu la torati 14 inazungumzia zaka ya pili, sio ya pili kusoma hili, mtu ajifikiriaye vizuri hulipata ombo. Kwanza hakuna popote katika biblia mwandishi anapata maneno “zaka ya pili” hata kama anayaangalia makala muhimu katika strong’s exhaustive concordance. Manano haya ni dawa ya kujitengenezea inayojaribu bila fanaka kuelezea kinaganaga maagizo kuhusu zaka katika nyakati za Musa. Pili, kama andiko hili lingezungumzia zaka ya pili kwa nini Musa alikuwa anawakumbusha wasomi mara mbili katika mistari ya 27 na 28 bila kusahau mlawi aliyepokea zaka ya kwanza. Kwa hivyo kupokea kutoka kwa zaka ya kwanza mlawi hangehitaji sehemu inayoitwa zaka ya pili. Kumbukumbu 14 inazungumzia kuhusu zaka ya kwanza na ya kipekee. Tatu kama makanisa yanaamini udanganyifu wa zaka ya pili kwa nini wasitengeneze nafasi katika bahasha za matoleo kwa mhisani kusihi zaka yake itolewe kama ya kwanza au ya pili. Zaka ya pili inafanya kama kizuia moshi ambayo matokeo yake ni kuchanganyikiwa wala sio ufafanuzi.



NI NINI KAPAUMBELE CHA KANISA LAKO?

Sasa wacha tufanye marudio ya haraka kuhusu jinsi kanisa inayotimiza mahitaji ya wajane, kukiwa na maskwota. Ni makao mangapi wajane makiwa na maskwota yanayosaidiwa na kanisa katika kijiji chako? Kama ungejibu hakuna hata moja kwa moja ya maswali haya kwa nini hayapo?

Kwa upande mwingine ni makanisa mangapi yanayofanya kazi katika kijiji chako? Mengi bila shaka! Ni viongozi wangapi wa injili wa kulipwa waliopo pengine asilimia 99.9 yana wahubiri au wazee wa kanisa.

Yawezekana kuwa makanisa mengi ya kikristo hayaendeshi makao ya makao ya wajane au maskwota vijijini mwetu kwa sababu ufadhili mkubwa katika makao makuu ya kanisa unatumika (i) kujenga upya (2) kulipia mishahara, nyumba, gari za kisasa masomo na nauli za viongozi wa kanisa?

Kama aya tatu zilizotangulia zinazungumzia jamii yako na kanisa si ni wakati wa kubadili kipaombele cha Mungu katika kumbukumbu 14 na Matayo 25?

Wakati Waisraeli walipofuata maagizo katika Kumbukumbu 14 – 11 kutimia zaka kusheherekea Baraka ya Mungu kwa mtoa zaka na familia yake na kudidhia Walawi na mahitaji mengine mtoe zaka alihakikishiwa baraka za Mungu na bidii yake.

Je ni nini kipaumbele cha kanisa lako? Tusaidie ulaji wa kikanisa au mahitaji ya binadamu?



MAFUNDISHO YA MALAKI KUHUSU ZAKA

Kabla kuacha suala la kutoa zaka katika agano la kale, wacha tusome Malaki kwani ni katika kitabu hiki viongozi wa kiroho wa kikristo hufundisha uongozi wa kikistro.

Hapana shaka umehudhuria mahubiri juu ya zaka na ukaambiwa na mhubiri kuwa kama hautalipa zaka kwa kanisa la mhubiri basi ‘unamwibia’ Mungu. Wacha tusome kitabu cha Malaki tuone ni kipi mtabiri anasema.

Sura ya kwanza inaanza pale Mungu anapowahakikishia Waisraeli kuwa anawapenda. Ndipo katika fungu 6 – 8 Mungu anasema “Ni nyinyi wahubiri muonyeshao madharau kwa jina langu” mhubiri anauliza “Ni vipi tumedharau jina lako? (NIV), Mungu anajibu munaweka chakula kilichonajisiwa katika madhabu yangu kwa kuleta wanyama vipofu, viwete na wagonjwa ‘fungu 9’ anarudia haya katika fungu 13 Mungu anaonya kuwa hatakubali kafara hizi duni (New Century Version). Tena katika fungu 14, Mungu anaona hili.

Katika sura ya pili Mungu anawazungumzia wahubiri akiwaambia kuwa wamefundisha taifa kutenda mabaya. Mabaya haya bila shaka yalijumlisha wahubiri kutotilia mkazo umuhimu wa watu

(1) Kuhakikisha haya mahakamani na (2) Umuhimu wa zaka na toleo la kafara isiyo chachu kwa Mungu (fungu 7 - 9).

Katika sura ya tatu Mungu anasema kwa nini amekasirika. Shida ni ipi? Tena wahubiri wanaweka kafara nzuri na siha huku wakitoa wanyama viwete, vipofu na wagonjwa kama kafara kwa Mungu na wahitaji walio na sehemu ya zaka. Mungu anawalaani wahubiri kwani katika sura ya 3:5, anasema, “nitashuhudia tena wale wanaodanganya wajane na yatima. Na nitashuhudia ya wale wanaowadhulumu wengine (New Century Version).

Kumbuka kuwa pamoja na walawi, makundi haya matatu ya wahitaji ndiyo yaliyohidhinishwa kupokea zaka katika Kumbukumbu la torati, sura ya 14.

Kwa hivyo shida iko na wahubiri walio walafi na wanaomnyanganya Mungu kafara njema na wahitaji chakula kizuri kiletwacho kama zaka na wakulima.

Sura ya 3:8 inauliza; “binadamu atamuibia Mungu?” Wahubiri wanataka kujua walivyomwibia Mungu. Mungu anajibu “kwa zaka na matoleo”. Kwa sababu hiyo, ghadhabu ya Mungu ni kupitia kukosana, wahubiri wamejiwekea yaliyo mema! Wahubiri ni wezi! Sura ya 9 inapendekeza kuwa sio tu kuwa wahubiri wamemwibia Mungu lakini pia kuwa wameliibia “taifa nzima” kwa kumfanya Mungu kukatalia baraka zake kwa watu wake. Kwa kuongezea watu kuwaona wahubiri wakijiwekea yaliyo bora na kuiga ulaji wa wahubiri walileta wanyama duni kwa Mungu pia.

Kwa hivyo ni wazi kuwa Mungu hazungumziii swala la kukatalia zaka na matoleo kabisa anawazungumzia wale wanaojiwekea wanyama bora badala ya kumtolea Mungu na kuwapa masikini.

Kwa hivyo Mungu anamzungumzia nani? Anawazungumzia wahubiri na waliomwibia Mungu na masikini kwa kujiwekea wanyama bora, (kutilia mkazo ni kwangu) kwa mfano, wahubiri waliwafundisha watu kuwa walafi. kwa hivyo, wakati mwingine mhubiri wako akisoma Malachi 3:8 na kuwanyoshea kidole kumbuka haya ni wazi kuwa mnatakikana kumnyoshea kidole.

Kiongozi yoyote wa kanisa akiharibu maagizo ya Biblia kwa kujinufahisha kidole cha lawama ya Mungu hunyooshewa yeye kwani sio mkusanyiko anaodai kuongoza kwa njia za Mungu (Malaki 2:8).



SURA YA PILI

FUNDISHO LA AGANO JIPYA

KUHUSU KUTOA ZAKA



Matayo anataja zaka katika sura ya 23:23. Yesu aliwakashifu viongozi wa wayahudi kwa kutilia mkazo zaka bora huku wakisahau “maswala muhimu, huruma na uaminifu”. Wafarasayo ambao Yesu alikuwa akiwazungumzia walikuwa kwa wakati huu chini ya sheria za Musa, kwani kifo cha Yesu hakikuzimaliza tu hizi. Tunasoma haya zaidi pale tunapofuka kwa maandisi ya Paulo.

Tena, hakuna rekodi kuwa Yesu au watumwa walikubali zaka kwao wenyewe. Tulivyoona katika Kumbukumbu la Torati 14 kutoa zaka lilichukuliwa kuwa nafsi ya mkulima kusherehekea na kumshukuru Mungu kwa baraka zake, sherehe ilikuwa kati ya Mungu na mkulima.

Hata hivyo vile agano jipya linavyoandikisha, Yesu na wafuasi ake walijitolea kwa kuwalinda masikini wenye njaa, wagonjwa na wahitaji.

Yesu aliwezaje? Akiwa mototo wa seremala? Yawezekana alifanya kazi kwa mikono yake, tunajua kuwa Yesu alifadhili kupita kwa kujitolea kutumia zawadi za marafiki (Luka 8:3) tena Yesu alikubali kupewa na marafiki, kwani katika Matayo 10 na Luka 10, alituma watumwa, akiwaambia kuchukua tu nguo walizovaa na kusema kuwa, “mfanyakazi apewe anachohitaji mshahara wa kila mara kutoka kwa zaka ya mkusanyiko, wakati tunakubali zawadi za kujitolea, mtu husema (kama unaweza kunipa kitu fulani kunisaidia katika kazi yangu ya kikristo, na kama anahitaji usaidizi, nitaukubali huo usaidizi. Ingawa kama hunaweza kunisaidia naamini Mungu atanipa. kwa hivyo kwa wema wa Kristo nitaendelea kukuhudumia!) Mfano mwafaka wa kutoa na kupokea unapatikana katika fumbo la Kristo la msamaria mwema Yesu aliwaambia wafuasi wake waige mfano wa msamaria mwema na wasidai malipo.

Kitendo kisicho cha watumwa cha kukodi kiongozi wa kiroho chaonekana kuwa na mizizi yake katika nasaha ya kikatoliki kuwa lazima kuwe na binadamu mpatanishi kati ya binadamu na binadamu na huyu awe mhubiri, sio Kristo. Paulo anasema wazi kuwa kuna mpatanishi mmoja tu , naye ni Yesu. Kwa bahati wakati waprotestanti walipoondoka kwa kanisa ya Katoliki walikataa kifungu hiki, kwa bahati mbaya, hawakukataa kile cha kulipa mishahara kwa wahubiri. Alexander Campbell anasema vizuri: kuajiri watu kuhubiri kwa mkusanyiko wa kikristo ni kinaya juu ya mkusanyiko uliowaajiri ………… ndio yeyote alipwaye kuhubiri …………… naamini ni utamaduni wa upuniaji, (1830, imenukuliwa katika ‘Examiner’, Sept. 1993). Hakuna nakala ya agano jipya ambapo Yesu au watumwa wake walikubali mishahara na marupurupu kwa kazi yao. Kwani wao sio mifao yetu? Je, tusaidie ulaji wa kikanisa au mahitaji ya kibinadamu?



BAADA YA MSALABA

Sasa tutasoma kama ua la zaka inaagizwa baada ya kifo cha Yesu msalabani.

Wakati Kristo alisulubishwa kitambaa cha hekalu kiliraruka kuashiria kuwa sheria za Musa zimekwisha, Paulo alizungumzia jambo hili kwa kusema kuwa mahitaji ya sherehe kama “nyama” na “vinywaji” siku takatifu na sabato ya sherehe havikuwa na maana baada ya kifo cha Kristo, kafara kuu, (Wakolosai 2:16, 17na Waibirania 9:8-11).

Kwa sababu kutoa zaka kulikuwa sehemu ya sheria za Musa na kwa sababu hili lilimalizwa na kifo cha Kristo si mahitaji ya zaka yangekataliwa pia? Ndio, kutobadilika kama vile na (kumbukumbu la torati 12:1-6).

Zaka, tohara na sherehe za kuosha, wanyama kuteketezwa n.k zilikomeshwa na kusulubishwa kwa Yesu (Wagalatia 5:6; 6:15; na Korinto 7:19).

Kwa sababu Paulo ni mfano wa pili wa Kristo katika Agano Jipya ni mkristo anayefaa kama mfano na kielelezao kwa mkristo wa kisasa.

Kwanza hakuna ushahidi wa Biblia kwamba Paulo alikubali zaka mwenyewe. Anajisifu kwamba ameifanya inchili bure kwa Wakorinto (1 Wakorinto 9:15) ni mara ngapi umesikia mhubiri akihubiri zaidi ya fungu la 14? Kwa nini wanasimamia fungu la 14 inawezakuwa ni kwa sababu Paulo katika fungu la 15 – 18 anaeleza vile hawezi kukubali mshahara kwa kazi aifanyayo. Mshahara wa Paulo ni furaha apatayo kwa kuwahudumia wakristo kwa moyo wake (1 Wakorinto 9:15-27).

Paulo anaandika katika fungu la 8 kuwa aliwaibia kanisa kwa kuwasaidia kwa kupokea msaada.

Katika kigiriki tunaona kuwa jina kusaidia katika tafsiri nyingine ni mshahara. Kwa hivyo Paulo alipokea vyakula vilivyopikwa kutoka kwa marafiki kwa hizani.

Jina kusaidia limetumika kwa sababu zifuatazo: -

(a) Paulo anaelezea vizuri katika Wakorinto wa kwanza kuwa alipeana injili bila malipo.

(b) Kam alipokea mshahara aliohitaji mbona aliwaambia Wakorinto kuwa liibia kanisa zingine ili kuwatumikia wao. Paulo alikubaliana na zawadi na wala si mshahara.

(c) Mambo ya chakula kilichopikwa katika mafundisho ya Paulo yanaonyesha kukubaliana na zawadi za kujitolea kama vile Yesu alifanya.



Yeyote atakayehubiri ya kwamba Paulo alihubiri kinyume atakuwa anajipendekeza mwenyewe wala Paulo hakupokea zawadi tu bali alifanya kazi kwa mikono kupata riziki? (Matendo 20:34) ni nini la mwisho ulimwona mchungaji wako akifanya kazi kwa mikono yake kusaidia huduma, (2 Watesolonike 3:6 - 13). Paulo anasema alifanya kazi usiku na mchana ili asile chakula cha watu bila kulipia na huu mfano wa kufanya kazi unastahili kwa wote 1 Wakorinto 11:1 “Mnifuate mimi kama mimi ninavyomfuata”.

Paulo ni mfano mzuri wa mkristo mzalishaji mali, mwenye furaha na kujitolea, kwa kiongozi yeyote wa kiroho kupata riziki kwa kujitolea bila kuitisha zaka ndio usimamizi halali.

Kumbuka kwamba baada ya msalaba hakuna ushahidi wa Biblia kwamba Paulo au wafuazi wa Yesu walipokea wala kutoa zaka. Paulo anakubaliana na Kristo kuwa wafanyakazi wa kiroho wapokee vipawa. Matendo 18 – Paulo anaelezea kuwa waliishi na Aquila ana Priscila wakifanya kazi ya kushona hema. Pia walikutana na Yusto mcha Mungu akamkaribisha.

Hakuna mahali katika Biblia ambapo Paulo au Yesu alifundisha kuwa wahubiri wapokee mishahara. Je tuunge ulaji wa kikanisa au ulaji wa kibinadamu?

Yatarajie mengi.



SURA YA TATU

KUTOA KWA MAKUANI WAKUU



Tumeona kwamba mtindo wa sherehe katika agano la kale ulimalizwa wakati Yesu alifuka kwa ajili ya dhambi zenu. Yaliokataliwa na mtindo huo ni pamoja na: - makuani wa kwanza, tohara, zaka, wanyama kuteketezwa na sherehe za kufua n.k.

Katika kujitolea kwake Yesu Myaudi alifanyika kuani mkuu, Waeberania 7, Paulo anaonyesha kuwa makuani wa kwanza walikufa na badala yao makuani wengine wakachukua usukani. Melizedeki mkuu wa amani (fungu 2) na uzima (ambaye Abraham alipeana zaka kwake) ni kioo cha kuani mkuu Messiah Kristo aliye na uzima. (Fungu la 5) inasema kuwa Mlawi aliyefanywa kuani angepewa amri ya sheria za shelee kupokea fungu la kumi la nyongeza ya mkulima. Ingawaje tumeona sheria za sherehe zilikomeshwa na kufa kwa Yesu, hakuna mchungaji ambaye atajiondoa kwa wenye dhambi kama yeye si mtakatifu. Weabrania 8:1 na 6 inamtoa Yesu kama kuani aketiye kitini cha enzi akihudumu kama mpatanishi mkuu.

Biblia inasema wazi jinsi ya kumpatia kuani wetu Mathayo 25:34 Kristo anasema atatawanya kondoo na mbuzi, watakatifu kutoka kwa wabaya, kondoo atawakaribisha mkono wake wa kulia katika ufalme. Ndiposa Mungu atawaelezea kwa nini atawakubali waliokoka; nilikuwa na njaa mkanilisha, nilikuwa na kiu mkanipa maji, nilikuwa bila makao mkanipa, nilikuwa uchi mkanifisha, nilifungwa mkaja kuniona.

Ndiposa watakatifu watauliza “Ni lini tulikutendea haya?”(fungu 40) Ikiwa umemmfanyia mwenzako umenifanyia mimi. Je ni njia gani tunampa kuani mkuu? Ni kwa kuwasaidia ndugu na dada zetu wenye mahitaji.

Kwa hivyo hatumpi yesu kwa kutuma zaka zetu kwa maofisi ya kanisa ambapo hupokelewa na wasio walawi na kutumia kama mishahara yao na ujenzi.

Angalia kusaidia walio na mahitaji kwa kutoa chini ya mapato yako katika mpangilio wa walawi wa zaka unaweza kuwa juu ya mapato yako.

Wakati wa Musa, lilikuwa utawala wakati watu walitoa kwa kanisa walito utawala. Leo hii kanisa ni tofauti na utawala. Katika Amerika. Asilimia 45% uenda kwa utawala kwa kanisa zaka ni 10% na asilimia 0.5% inaenda kwa wasiojiweza makao ya myatima wanapeana 60% kwa manyumba yao. Ni wazi kwamba asilimia 40% ya mapato yalibakia wafanyikazi, walawi katika wakati wa Musa walikuwa 60-70% ya mapato yao hubakia kwa matumizi yao. Wakristo wengi hawako macho kama vile kwa siasa.

Siku hizi baada ya Yesu kutukomboa tunapeana kwa kuwani Mkuu kwa kuwalinda wenye mahitaji. Je kanisa lako linatilia maanani kusaidia wenye mahitaji au ni kununua mashamba kujenga nyumba. Kuna viongozi wa kanisa wanaosema kwamba.

Kujenga manyumba mapya kunaonyesha “kukua kiroho”

Hakuna mahali yesu amelinganisha ujenzi wa kanisa na ukuaji kiroho. Anasema analinganisha ukuaji kiroho kwa makadilio ya sisi kulinda wajane, yatima, walio na kiu, wasio na makao na walio njaa.

Kutumia makadilio ya Yesu kanisa lenu limefanya mazuri kufika wapi? Je tuunge ulaji wa kanisa au alaji wa dini?

(Yatarajie mengi)



SURA YA NNE

NAFASI YA MADALIKO KANISANI

Kulingana na ushahidi ulijitokeza juu ni kwamba bado kanisa zingine zachukulia sheria za sherehe za kutoa zaka ya fungu la kumi kila mwaka kwa lazima> Ingawaje hii ni nafasi ya ufalisayo na tunaangalia juu yake tutilie maanani kidogo:

Kama kweli sheria za sherehe hizi bado zafuatiliwa mbona kanisa zingine hazifuatilii mambo yanayolingana na sherehe kama:-

1. Makuani wa walawi hawakuruhusiwa kurithi shamba. Hizi kanisa huwazuia wahubiru kurithi mali?

2. Kumbukumbu la torati 14, lasema kuwa fungu la kumi liende malango ya mkulima ili yalishe yatima wajane wageni pamoja naye mkulima na familia yake.

Je umewahi kusikia muhubiri akisema kuwa kutumia fungu la kumi waumini mulisha familia zenu?

3. Hawali katika siku za malaki makuani waliokuwa na tamaa walijichukulia mazao mazuri kwanza na kupeana mazalio kwa Mungu na amskini. Bado Mungu siku hizi huwalaani wachungaji wanaojipatia mshahara mzuri ilhari wanaosumbuka kwa jamii bila mahitaji ya kimsingi wapo?

4. Kikristo kulingana na kazi ya wachungaji wa sasa makuani wakati wa Musa ni ufalisayo mtupu. Makuani wa agano la kale walitoa sadaka ya keteketezwa na kuwa wapatanishi kati ya Mungu na wanadamu. Siku hizi wachungaji huwahudumu kama wapatanishi wala kutoa sadaka. Kristo pekee ndiye mpatanishi wa uzima aliyeketi mkono wa kulia wa Mungu aliyejitolea kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu.

5. Ni makuani wa walawi pekee waliostahili zaka mchungaji wako ni wa kabila la walawi?(Hesabu 3)

6. Kanisa lafunza kuwa kila mapato yatolewe katika fungu la kumi lakini walawi 27 yasema kuwa ni mapato ya shamba na matunda ya miti yangetolewa zaka. Amri hii iliwaweka nje waashi wavuvi,wanaoshona nguo, viatu na mikeka n.k. Ni bayana kuwa mkristo wa kawaida kanisani anatengeneza pesa kuliko kuhubiri ukweli neno la Mungu.

7. Walawi walitakiwa kuleta zaka yao ya chakula wala si pesa. Kama wangeleta pesa walikuwa wanatoa asilimia ishirini 20% juu yake- walawi 27:30. Vile tumeona wakristo wa kisasa hawaja acha kufuatilia sheria za sherehe mzima. Kanisa lataka waumini kufuata kipande kimoja kinachowaezesha kuwa tajiri na kupokea mishahara mizuri. Je tuunge mkono tamaa ya makanisa au tamaa ya wanadamu?



SURA YA TANO

MIFANO YA UKWELI KATIKA MAISHA



Ilikuwa mwezi wanne na jua kali mhubiri Smith (protestant) alikuwa akiendesha gari na nduguye Brown mkuu wa Deacon mbele ya masaa matatu kanisani ya mkutano wakawa wanacheza mpira wa golf huu mkutano ungekuwa wa maana na mada kuu zilikuwa; (1) jinsi ya kupata pesa za kuongeza kanisa mpya iliyoko Riverside Drive.

(2)Kumuadhibu Deacon wa kanisa, huyu Deacon alikuwa akitumia pesa za kanisa kwenda kwa yatima wa salvation army badala ya kutumia pesa kanisani zifanye mipango ya kanisa. Haya ndiyo yaliyokuwa mashtaka yake.

Kama wanaendelea kucheza simu yake mhubiri Smith ikali. ”Hello” alisikia mwanamke kutoka upande mwingine wa simu akisema hana makao anasafiri kwenda Baltimore kutoka Charlotte ambako watakaa na mototo wake wa miaka mitatu hadi apate kazi.Gari lake la aina la 1981 Honda ya huyu mwanamke lilikuwa linahitaji pauni 38 zilizobaki kutengeza radiator ambayo ilikuwa inatakiwa pauni 74.39 Aliangaika na kushindwa kama mchungaji huyu atampa usaidizi wa kupata radiator nyingine kwa kumuongezea pesa anunue mpya.

Mhubiri kumjibu alimwambia ya kwamba yu garini akisafiri kwenda mkutano na Deacon mkuu hangeweza kumsaidia ampigie simu keshowe atapata wakati wa kuongea naye aone kama katika matumizi ya kanisa kungepatikana na pesa za kukomboa nyumba. Hata hivyo alimshukuru kwa muda aliompa.

Huyu mwanamke aliangalia upande mwingine na kuona mwanamke wa salvation Army volunteer aliyekuwa akitengeneza gari yake. Alimweleza shida yake akakubali kumsaidia kumtengenezea gari lake kwa garage. Kumchukua na mototo wake awape chaakula na mahali pa mapumziko ndiposa waendelee na safari yao ikiwa vizuri.

Kati ya hawa wakristo ni nani atapata Baraka za Mungu akirudi kuwatawanya kondoo na mbuzi. Ni shirika lipi latoa kwa kristo aliye kuani mkuu? Kulingana na hadithi hii ni mhubiri Smithh au ni kijana wa Salvaton Army? Tuunge tama ya makanisa au tamaa ya ubinadamu?



MARUDIO KATIKA NJIA YA MUHTASARI

Tumejifunza kutoka kwa bibilia kuwa :-

a) Zaka ilihitajika kulingana na sheria za walawi

b) Zaka, fungu la kumi ilikuwa nyongeza ya mapato ya mtu

c) Zaka ilitumika kusheherekea Mungu vile vile kusaidia walawi waliokuwa wajane yatima na wasio na makao.

d) Wakati mwingine makuani walipuuza zaka kwa kujiwekea vinono na kutojali wanyonge/ maskini.

e) Baada ya kusulubiwa na kufa kwa Yesu msalabani kwa ajili ya dhambi zetu sherehe za kisheria ikiwepo tohara na zaka ziliwekwa kwa lazima kila mwaka.

f) Paulo, watumwa na Kristo mwenyewe alikubaliana na kupewa zawadi kutoka kwa marafiki.

g) Katika bibilia hakuna mahali tunaona kuwa Paulo, watumwa na kristo walipokea zaka wala kutoa wala kutegemea zaka kwa kuwalisha.

h) Mtindo wa sherehe wa makuani kutoa sadaka kuteketezwa ulimalizwa na kuani mkuu aketiye kitini cha enzi akihudumu kama mpatanishi mkuu kati yetu sisi na Mungu.

i) Yesu anatwambia kuwa ikiwa twataka kuhesabiwa wenye haki arudipo mara ya pili lazima tuwahudimie maskini wasio na makao na waliofungwa

Kwa baati mbaya wakristo kanisani wameamua

1. Kupuuza mafundisho ya Paulo

2. Kuwalipa wachungaji mishahara mikubwa kutokana na pesa za waliokufa.

3. kutofanya kazi hili wajisaidiea wasiojiweza kama Kristo na Paulo ambao wanatumika kama mifano mizuri katika kanisa la leo.





Tabia ya kutoa zaka na sheria za sherehe, kanisa kukubaliana mambo haya sherehe zilizokufa na kwa kufanya hivyo wanakataa damu ya Yesu mkombozi na mpatanishi wetu.

Kwa wasimamizi wa kanisa kupuusilia mafundisho ya bibilia ni tendo ambalo haliwezi kuepukika na wasimamizi wanaodai kuwa wanaelekeza wafuasi wao kwa njia ya kweli kulingana na mafundisho ya bibilia.

Ikiwa unatoa zaka au kupokea zaka utafanya nini na kwel? Jibu lako kwa swali hili bila shaka litakuwa na matokeo ya uzima!

Mungu akupe nguvu ya kusimama na ukweli vile unaejitahidi kulisha kondoo, kufuata neno lake na uhesabiwa katika watoto wake katika kurudi kwake mara ya pili.



MFANO WA KUMALIZIA

Si kitambo sana mchungaji an kristo walikuwa wanatembea kijijini cha mtaa mmoja. Katika mlango wa nyumba iliyoamwa kulikuwa na kijana wa miaka saba aliyevaa nguo chafu kijana aliwaangalia Yesu na mchungaji. Alikuwa na nywele ndefu, chafu nguo zilizoraruka na viatu vilivyoisha na miguu kutokea nje. Mchungaji alimuuliza Yesu mbona unaharibu wakati kwa mtu asiyefaa? Yesu alimwangalia mchungaji na kumjibu “Ni mimi niliyekuumba wewe na ni mimi niliye muumba huyu ndugu”



SWALI LA MWISHO

Je wewe na kanisa lako mtaendelea kuhesabu ufanishi kwa kuongezeka kwa watu kanisani, nyumba, nyongeza ya zaka mishahara ya utumizi au wewe na kanisa mtatoa mliconacho kwa chokora?

Kumbuka ni Yesu aliyemwita chokora nduguye! Utafanya nini na nduguyo mkombozi wako?

Utafanya nini na huyo mototo? Mwishowe, Utafanya nini na kristo?



Kwa mengi zaidi wasiliana na :-

Daktari Fillimer Hevener
(434) 392-6255
E-mail

COPYRIGHTED 2001,
BY FILLMER HEVENER
224 MOHELE ROAD
FARMVILLE, VIRGINIA  23901
(434) 392-6255)


(All rights Reserved. No portion of this document may be reproduced in any way without the written consent of  Fillmer Hevener.  Please email him for written permission to reproduce this article.)


 

 Â© 2005 Guthrie Memorial Chapel